• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Benki ya CRDB yakabidhi Madawati 40 yenye thamani ya shilingi million 4 kwa Sekondari ya chitekete

Posted on: August 4th, 2025

Benki ya CRDB kupitia Tawi la Newala imekabidhi madawati 40 yenye thamani ya shilingi milioni 4 kwa Shule ya Sekondari Chitekete, iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Newala mkoani Mtwara, kupitia mpango wake wa kijamii wa “Keti Jifunze”. Msaada huo umetolewa kwa lengo la kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi, huku ukilenga kupunguza changamoto ya uhaba wa madawati mashuleni.


Mpango wa Keti Jifunze ni moja ya mikakati ya Benki ya CRDB ya kusaidia maboresho ya elimu kwa shule za serikali kwa kutoa viti, meza na vifaa vingine muhimu vya kujifunzia. Mpango huu ni sehemu ya mchango wa benki hiyo katika kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita ambayo imeendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika sekta ya elimu, hususan miundombinu na vifaa vya kufundishia.


Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo katika Hafla iliyofanyika tarehe 1 Agosti 2025 Shuleni hapo, Meneja Biashara wa CRDB Kanda ya Kusini, Bw. Emmanuel Biganio alisema mpango wa Keti Jifunze umefikia awamu ya tatu na unalenga kutoa madawati katika halmashauri 185 nchini kote. Kwa Kanda ya Kusini pekee, zaidi ya madawati 450 yanatarajiwa kusambazwa kwa shule zilizochaguliwa, ambapo Sekondari ya Chitekete ni miongoni mwa walionufaika.


 “Sisi kama wadau, kama wananchi wa Tanzania na taasisi inayofaidika na utulivu wa nchi hii, hatuwezi kukaa kimya. Kupitia taasisi yetu, tumeamua kuchangia maendeleo haya kwa kutoa madawati kwenye shule za serikali, tukianza na halmashauri 185 nchini kote,” alisema Bw. Biganio.


Msaada huo ulipokelewa rasmi na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Bi. Magreth Likonda, ambaye aliishukuru benki ya CRDB kwa kuonesha mshikamano na ushirikiano wa dhati na serikali katika kuleta maendeleo ya elimu kwa vitendo. Alieleza kuwa msaada huo utachangia kuongeza ari ya walimu kufundisha na wanafunzi kujifunza katika mazingira bora zaidi.


Hafla ya kukabidhi msaada huo ilihudhuliwa na Viongozi Serikali ya Kijiji cha Chitekete , Wananchi,Walimu na Maafisa Elimu ngazi ya kata na Halmashauri.

@mtwarars_habari 

@ortamisemi 

@msemajimkuuwaserikali 

@gersonmsigwa 

@samia_suluhu_hassan 


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Benki ya CRDB yakabidhi Madawati 40 yenye thamani ya shilingi million 4 kwa Sekondari ya chitekete

    August 04, 2025
  • SALAMU ZA SHUKRANI KWA RAIS SAMIA

    July 24, 2025
  • MAPOKEZI YA FEDHA KWA MWAKA 2025/2026

    July 24, 2025
  • MAPATO YA NDANI KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025

    July 24, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Kitangari,Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa