• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala lapitisha makadirio ya bajeti ya shilingi bilioni 17.3 kwa mwaka wa fedha 2019/2020

Posted on: February 14th, 2019

Mkutano wa baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala wapitisha makadirio ya bajeti ya shilingi bilioni kumi na saba, milioni mia tatu ishirini na nane na elfu tisini na tano (17,328,095,000.00).

Akiwasilisha kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Juma Rahisi ameeleza kuwa, kwa mwaka  wa fedha 2019/2020, Halmashauri kupitia vyanzo mbalimbali vya mapato ikiwemo ruzuku kutoka Serikali kuu, wahisani wa maendeleo na mapato ya ndani ya Halmashauri imekadiria kukusanya jumla ya shilingi 17,328,095,000.00 ambayo itatumika katika kuhudumia sehemu kuu tatu ambazo ni mishahara ya watumishi, matumizi ya kawaida ya uendeshaji  wa ofisi za Halmashauri na kugharamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Bw. Rahisi alieleza kuwa mapato kutoka Serikali kuu yanakadiriwa kuwa kiasi cha shilingi 15,519,796,000.00, wahisani wa miradi ya maendeleo shilingi 375,679,000.00 na mapato ya ndani shilingi 1,432,620,000.00.

Halmashauri ya Wilaya ya Newala kwa vyanzo vyake vya ndani imekadiria kukusanya mapato yenye thamani ya shilingi 1,073,800,000.00 kutoka vyanzo vya mapato halisi na shilingi 358,820,000.00 kutoka vyanzo vya mapato lindwa ambavyo ni mfuko wa elimu, ada ya wanafunzi kidato cha 5 na cha 6, gharama za mfuko wa afya ya jamii, bima ya afya, malipo ya papo kwa papo na mfuko endelevu wa dawa (DRF).

Makadirio hayo ya makusanyo ya mapato ya ndani ni pungufu ya  shilingi 489,647,000.00 ya makadirio ya bajeti ya mwaka 2018/2019 ambayo ilikuwa ni shilingi 1,922,267,000.00 sawa na upungufu wa asilimia 34.

Akiendelea kuzungumza kwenye baraza hilo la madiwani, Bw. Rahisi alifafanua kuwa kuna sababu mbalimbali zilizopelekea kushuka kwa makisio ya mapato ya ndani kwa mwaka 2019/2020 ambazo ni kukosekana kwa masoko ya mazao mchanyanyiko, uwepo wa makadirio makubwa kwa baadhi ya vyanzo kuliko hali halisi ya makusanyo, kuyumba kwa makusanyo yatokanayo na mfuko wa elimu na kubadilika kwa mfumo wa ununuzi wa korosho.

Mkuu wa Wilaya ya Newala Bi. Aziza Mangosongo (aliyesimama) akizungumza kwenye mkutano wa baraza la madiwani la kupitia rasimu ya bajeti ya Halmashauri ya mwaka 2019/2020

Akizungumza katika baraza hilo, Mkuu wa Wilaya ya Newala, Bi. Aziza Mangosongo, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Newala kwa kuendelea kubuni vyanzo vipya vya mapato ambapo kwa sasa imeanzisha kituo kikubwa cha mabasi katika eneo la kitangari ambapo mabasi yote yanayofanya shughuli za usafirishaji wa abiria na yanayopita katika eneo la kitangari yanatakiwa kuingia, kupakia na kushusha abiria katika kituo hicho na kulipa ushuru hivyo kuipatia mapato Halmashauri.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa M. Chimae (aliyesimama) akitolea ufafanuzi hoja zilizoibuliwa  kwenye mkutano wa baraza la madiwani la kupitia rasimu ya bajeti ya Halmashauri ya mwaka 2019/2020

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Bw. Mussa Chimae, amewaeleza wajumbe wa baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Newala kuwa Halmashauri kwa sasa imedhamiria kuongeza zaidi mapato kwa kuibua vyanzo vipya vya mapato na kuboresha vyanzo vya zamani. Na hili linajidhihirisha kwenye uanzishwaji wa kituo kikubwa cha mabasi katika eneo la kitangari, ujenzi wa mabanda ya biashara kuzunguka kituo hicho, uanzishwaji wa kituo cha kupimia na kuuzia korosho zilizobanguliwa eneo la Kitangari ambapo Halmashauri inapata ushuru kwenye biashara hiyo na uimarishwaji wa kituo cha redio Newala ambacho ni mali ya Halmashauri ili kuongeza wigo wa usikivu, kuboresha miundombinu na maslahi ya watumishi na kuvutia wateja mbalimbali kutangaza na redio Newala hivyo kuongeza mapato ya ndani yaHalmashauri.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Mhe. Chitwanga Ndembo (aliyesimama) akifunga  mkutano wa baraza la madiwani la kupitia rasimu ya bajeti ya Halmashauri ya mwaka 2019/2020

Akifunga mkutano huo wa baraza la Madiwani, Mwenyekiti wa  Halmashauri ya Wilaya ya Newala Mhe. Chitwanga Ndembo amewataka timu ya menejimenti ya Halmashauri kuyafanyia kazi mapendekezo yote yaliyotolewa kwenye makadirio ya bajeti ya Halmashauri kwa mwaka 2019/2020 ili kuboresha huduma kwa wananchi na maslahi ya waheshimiwa madiwani hivyo kuleta heshima kwa viongozi hao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI -HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA December 29, 2023
  • KUITWA KWENYE USAILII WA MAHOJIANO January 06, 2024
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2021 MNYAMBE SEKONDARI July 10, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 22, 2022
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AMEBORESHA SEKTA YA ELIMU NEWALA DC

    March 25, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA KINYWA NA MENO WAHUDUMIA WAGONJWA 319 NEWALA DC

    March 24, 2025
  • MIAKA 4 YA RAIS DKT. SAMIA SALUHU HASSAN AMEBORESHA HUDUMA ZA AFYA

    March 19, 2025
  • NEWALA DC YANUFAIKA NA JENGO LA UTAWALA,WATUMISHI

    March 18, 2025
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa