Baraza Maalum la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Newala, jana Februari 11, 2026, limejadili na kuidhinisha Rasimu ya bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 yenye jumla ya Shilingi bilioni 25.7, inayolenga kuimarisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuboresha huduma kwa wananchi wa Wilaya ya Newala.
Rasimu hiyo iliwasilishwa na Mkuu wa Idara ya Mipango wa Halmashauri, Bw. Sylvester Ngonyani, ambapo alieleza kuwa bajeti hiyo imezingatia miongozo ya Serikali, vipaumbele vya maendeleo vya taifa, na mahitaji halisi ya jamii katika sekta za elimu, afya, miundombinu na ustawi wa jamii.
Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala, Mheshimiwa Siwanina Jazari, alisisitiza umuhimu wa kuongeza ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kuwezesha utekelezaji wa bajeti kwa ufanisi. Alisema kuimarishwa kwa vyanzo vya mapato kutasaidia Halmashauri kutekeleza miradi ya maendeleo na kuongeza ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi.
Aidha, Mheshimiwa Jazari aliwataka Wakuu wa Idara na Vitengo kuhakikisha usimamizi madhubuti wa mapato, uwajibikaji wa watendaji, na matumizi sahihi ya rasilimali za umma. Alisisitiza kuwa ushirikiano wa watendaji ni msingi wa kufanikisha malengo ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa Wilaya ya Newala.
@tamisemi
@mtwarars_habari
@msemajimkuuwaserikali
@chikaladigitaltv
@dc_newala
Kitangari,Newala
Anuani ya Posta: P.O. Box 16
Simu: +255232410251
Mobile:
Barua pepe: ded@newaladc.go.tz
Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa