• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Newala District Council
Newala District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Newala

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
      • Chimbuko
      • Ukubwa wa eneo
      • Watu wa eneo husika
      • Shughuli za kiuchumi
      • Orodha ya viongozi
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Planning, Statistics and Coordination
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • KIlimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • ICT & Public Relations
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Usambazaji
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
      • TASAF
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba

Wilaya ya Newala yazindua maadhimisho ya wiki ya maji

Posted on: March 17th, 2021

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Mhe. Mfaume Ladda jana tarehe 16/03/2021 amezindua maadhimisho ya wiki ya maji Wilaya ya Newala kwa kushirikiana na wananchi wa Newala kufanya usafi wa mazingira na kupanda miti katika chanzo cha maji Mitema kilichopo katika kijiji cha Mitema, Halmashauri ya Wilaya ya Newala.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Newala Mhe. Mfaume Tamimu Ladda akizungumza siku ya uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya maji Wilaya ya Newala katika kijiji cha Mitema.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mhe. Ladda ameeleza kuwa wiki hii ya maji ina lengo la kujenga uelewa na kuhamasisha umma juu ya mipango na mageuzi yanayoendelea ya sekta ya maji na umuhimu wa ushiriki wa kila mdau katika mipango ya usafi wa mazingira na usambazaji wa maji. Hivyo kuwataka wana jamii kutunza mazingira katika vyanzo vya maji ili kuwa na huduma za maji endelevu.

"Katika kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi, Serikali ya awamu ya tano imefanya maboresho ya kuunda wakala wa maji na usafi wa mazingira Vijijini (RUWASA) ambao kwa wiki hii ya maji wamejipanga kupanda miti katika maeneo jirani na vyanzo vya maji; kufanya usafi katika maeneo ya matenki na vyumba vya pampu; na kufanya mafunzo kwa jumuiya za watumia maji na kuweka mawe ya msingi katika miradi ya Chitandi na Chiule." Alisema Mhe. Ladda

Wananchi wa Mitema wakishiriki kupanda miti katika maeneo ya chanzo cha maji Mitema siku ya uzinduzi ya maadhimisho ya wiki ya maji Wilaya ya Newala. 

Kwa wakati mwingine akizungumza katika uzinduzi huo, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Newala, Mhandisi Nsajigwa Sadiki, amesema kuwa maadhimisho ya wiki ya maji Wilaya ya Newala kwa mwaka huu 2021 yatajikita katika kuonyesha thamani ya maji katika nyanja za kijamii na kiuchumi yakienda sambamba na uzinduzi wa miradi ya maji iliyokamilika na uwekaji wa mawe ya msingi.

Meneja wa RUWASA Wilaya yaNewala, Mhandisi Nsajigwa Sadiki akizungumza na wananchi siku ya uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya maji Wilaya ya Newala

"Lengo kuu la kuweka mawe ya msingi katika maadhimisho ya wiki hii ya maji ni kutumia fursa hii kuonesha mafanikio ya Wizara ya Maji kwa vitendo na namna ambavyo huduma ya majisafi na usafi wa mazingira imeweza kuboreshwa nchini kwa kipindi kifupi." Alisema Mhandisi Nsajigwa.

Kila mwaka nchini Tanzania wiki ya maji huadhimishwa kuanzia tarehe 16 mpaka 22 mwezi Machi, kwa lengo la kuungana na mataifa mengine duniani katika kutathmini utekelezaji, mafanikio, changamoto na kuainisha mikakati ya kuboresha na kuimarisha utoaji wa huduma ya maji safi na usafi wa mazingira na kutunza usimamizi wa rasilimali za maji nchini.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya wiki ya maji kwa mwaka huu 2021 ni "Thamani ya maji kwa uhai na maendeleo."

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE KWA SHULE ZA HALMASHAURI YA WILAYA YA NEWALA January 15, 2021
  • MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021 December 23, 2020
  • KUITWA KWENYE USAILI December 02, 2020
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI November 13, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • Wilaya ya Newala yazindua maadhimisho ya wiki ya maji

    March 17, 2021
  • Mfuko wa elimu waendelelea kuimarisha sekta ya elimu Newala

    February 15, 2021
  • Uzinduzi wa Upandaji wa miti Mkoa wa Mtwara wafanyika Newala.

    February 13, 2021
  • Kamati ya Siasa Wilaya ya Newala yaridhishwa na utekelezaji wa ilani ya CCM Newala

    February 04, 2021
  • Ona Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Historia ya Halmashauri
  • Idara ya Rasilimali Watu

Kurasa mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Poralg
  • Secretariet ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Newala

    Anuani ya Posta: P.O. Box 16

    Simu: +255232410251

    Mobile:

    Barua pepe: ded@newaladc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma zetu

Hakimiliki@2016 Halmashauri ya Wilaya ya Newala. Haki zote zimehifadhiwa